Mil 177 kumng'oa Kichuya Simba - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Wednesday 15 November 2017

Mil 177 kumng'oa Kichuya Simba


Kichuya ni miongoni mwa wachezaji kadhaa ambao mikataba yao na Simba inaelekea ukingoni na mabosi wa timu hiyo tayari wameanza kuhaha kumshawishi aongeze kandarasi hiyo inamalizika mwishoni mwa msimu.

Kuna taarifa za chinichini zinaeleza kuwa winga wa Simba, Shiza Kichuya amegoma kusaini mkataba mpya klabuni hapo baada ya kupata ofa ya maana kutoka kwa timu moja ya Kiarabu.

Kichuya ni miongoni mwa wachezaji kadhaa ambao mikataba yao na Simba inaelekea ukingoni na mabosi wa timu hiyo tayari wameanza kuhaha kumshawishi aongeze kandarasi hiyo inamalizika mwishoni mwa msimu.

Hata hivyo kiwango kilichoonyeshwa na winga huyo tangu ametua Msimbazi na pia katika michuano ya COSAFA iliyofanyika Afrika Kusini mwezi Julai, kimempa ulaji kutoka kwenye timu hiyo kutoka ukanda wa Afrika Kaskazini.

Meneja wa mchezaji huyo Profesa Midundo Mtambo amedokeza kuwa wanataka mchezaji huyo akacheze soka la kulipwa nje ya nchi kwani itakuwa faida kwake (Kichuya) na Taifa zima.

No comments:

Post a Comment