Mc pilipili afunguka kuwa na mahusiano na mastaa hawa - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Thursday 9 November 2017

Mc pilipili afunguka kuwa na mahusiano na mastaa hawa

MCHEKESHAJI mahiri, Emmanuel Mathias ‘MC Pilipili’ ameweka wazi kuwa Miss Shinyanga na mshiriki wa Miss Tanzania 2014, Nicole Sarakikya na mwigizaji Rose Ndauka kwa nyakati tofauti ametembea nao lakini kwa sasa kila mtu ana maisha yake.

Pilipili alifunguka hayo hivi karibuni baada ya mwanahabari wetu kumtaka aweke ukweli juu ya warembo tofauti ambao anatajwa kuanguka nao dhambini akiwemo Nicole, Rose na msanii wa Bongo Fleva, Nandy.

“Nandy ni mshikaji tu hakuna chochote zaidi ya urafiki wa kawaida. Rose Ndauka na Nicole ni kweli nimetembea nao lakini wote siko nao kwa sasa, wamebaki kuwa marafiki wa kawaida tu,” alisema Pilipili.

No comments:

Post a Comment