POLISI WAMWACHIA PETER MSIGWA USIKU. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Monday 25 September 2017

POLISI WAMWACHIA PETER MSIGWA USIKU.

MBUNGE wa Iringa Mjini (Chadema) Msigwa ameachiwa huru jana usiku  kwa dhamana baada ya kukamatwa akiwa kwenye mkutano wa hadhara.

Msigwa ameachiwa baada ya kudhaminiwa na wadhamini wawili Alex Kimbe pamoja na Mwenyekiti wa Bavicha Iringa  Leonce Marto , saa nne usiku .

Msigwa alishushwa jukwaani kwa nguvu akiwa anahutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa na anatuhumiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya vyombo vya usalama.

No comments:

Post a Comment