Harmonize mpaka sasa hajatimiza ahadi ya Mil 10 za Shishi trump tatizo nini... - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Sunday 4 February 2018

Harmonize mpaka sasa hajatimiza ahadi ya Mil 10 za Shishi trump tatizo nini...

Kwenye sherehe harusi ya Msanii wa muziki Shilole baadhi ya wasanii walitoa ahadi nyingi na wengi sana walitoa ahadi lakini kulingana na taarifa za kamati ya ufatiliaji wa ahadi zilizotolewa siku hiyo hadi sasa 99.9% ya ahadi zilizotolewa siku hiyo hazijatimizwa na hakuna dalili yeyote ya ahadi husika kutimizwa....

Kati ya watu walio toa ahadi kwa Shilole na Mmewe ni msanii mmakonde Harmonize na Mzungu wake wa Arusha ambao kwa pamoja waliahadi kumnunulia Shilole gari yenye thamani ya Million 10 wakishaichagua wawambie hata kama ni leo au kesho...baada ya ahadi ile ukumbi ulilipuka kwa vifijo na nderemo kutokana na ahadi ya uhakika na ya haraka ailiyotoa Konde Boy.....

Baada ya harusi kamati ilibidi kuanza kufatilia ahadi za watu walio toa lakini kamati iliona ianze na ahadi ya msanii Harmonize ambayo ilionesha ni ya haraka sana na alionesha anataka kuitimiza haraka sana..... baada ya kupata aina ya gari walio hitaji wahusika kamati walimpelekea ujumbe Harmonize lakini hadi sasa Harmonize amepiga kimya as if si yeye aliyetoa ahadi ile na wala hajibu sms za wana kamati wala hatoi ushirikianoe

Kwakuwa ahadi ni deni wana kamati wamejipanga kuonana na uongozi wa Harmonize ili wajue watatimiza vipi hiyo ahadi aliyotoa msanii wao.....

No comments:

Post a Comment