Rais Mugabe ajiandaa kuondoka madarakani - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Wednesday 15 November 2017

Rais Mugabe ajiandaa kuondoka madarakani

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani saa chache baada ya jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka, kwa mujibu wa mtandao maarufu wa habari nchini Afrika Kusini.

"Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani," mtandao wa wa News24 uliandika bila ya kutoa taarifa zaidi.

Misukusuko ya kisiasa imekuwa ikiongezeka tangu Mugabe hivi majuzi amfute Emmerson Mnangagwa, mshirika wake wa miaka mingi kama makamu wa Rais.

No comments:

Post a Comment