Siri ya Raisi Magufuli kumpa Angellah kairuki wizara ya Madini. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Sunday 8 October 2017

Siri ya Raisi Magufuli kumpa Angellah kairuki wizara ya Madini.

Hizi inawezekana kabisa ndizo sababu kwanini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemteua na kumpa Angellah Kairuki Wizara mpya ya Madini.

1. Kutokana na kumudu vilivyo katika Ofisi aliekuwepo awali yaani Wizara -Ofisi ya Rais, Menejementi ya Utumishi wa Umma na Utawala bora.

2. Kutokana na Mh Kairuki kubuni mbinu mbalimbali za kuangalia upya mifumo ya ajira kwa kubuni uhakiki wa vyeti, uhakiki wa mifumo ya mishahara, ubunifu wa kupata taarifa za wafanyakazi halali na uhalali wa wafanyakazi waliopo na wale waliopo katika payroll yaani 'hewa' hali iliopelekea serikali kuokoa mabilioni ya shilingi.

Hiki ndicho kilichomsukuma kwa utashi na kwa imani alionayo kwa Mh Angellah Kairuki ndipo Mh Rais John Pombe Joseph Magufuli kumteua katika Wizara hii mpya ya Madini na Wizara ngumu iliowashinda wengi Ma- Dr na Ma- Professa hii itapelekea Angellah Kairuki ahakiki tena aina, na idadi ya migodi yote nchini kutokana na ubunifu na uaminifu alionao Mama huyu

No comments:

Post a Comment