WATU WASIO JULIKANA WAMEVAMIA OFISI ZA MAWAKILI WA MANJI. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Tuesday 12 September 2017

WATU WASIO JULIKANA WAMEVAMIA OFISI ZA MAWAKILI WA MANJI.

Polisi wakiwa eneo la tukio.
WATU wasiojulikana usiku wa kuamkia leo Septemba 12, 2017 wamevamia na kufanya uharibifu katika Ofisi za Wanasheria wa Prime Attorneys zilizopo eneo la Tambaza, jijini Dar es Salaam.

Milango ilivyovunjwa.
Inadaiwa kuwa watu hao wametoweka na kabati la kutunzia nyaraka na fedha. Mawakili hao (Prime Attorneys) kwa sasa wanafanya kazi ya utetezi katika kesi za mfanyabiashara Yusuf Manji.
Miongoni mwa mawakili wanaofanya kazi kwenye ofisi hizo ni wakili wa Manji Hudson Ndusyepo anayemtetea katika kesi zake zinazoendelea mahakamani

No comments:

Post a Comment