OKWI AELEZA JINSI ALIVYO FUNGA MAGOLI 6 KATIKA MECHI 2. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Sunday 17 September 2017

OKWI AELEZA JINSI ALIVYO FUNGA MAGOLI 6 KATIKA MECHI 2.

Baada ya kufunga mabao mawili wakati Simba ikiitwanga MWadui FC kwa mabao 3-0, Emmanuel Okwi amesema pamoja na juhudi, ushirikiano na wenzake ndiyo chachu ya mafanikio hayo.

Okwi raia wa Uganda amesema ushirikiano wake na wenzake umemfanya kufikisha mabao 6 katika mechi tatu za Ligi Kuu Bara.

“Ushirikiano na wenzangu ndiyo jambo namba moja zaidi, nimefanikiwa kufunga mabao mawili na kufikisha sita kwa kuwa tunashirikiana na wenzangu, nawashukuru.

“Kingine ni juhudi lakini pia kumuamini Mungu kutokana na ninachokitaka,” alisema.

Katika mechi ya kwanza ambayo Simba ilishinda mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting ambayo ilikuwa ya ufunguzi wa ligi, Okwi alifunga mabao manne.
Katika mechi ya pili, hakucheza wakati Simba ikitulizwa kwa sare ya bila kufungana dhidi ya Azam FC.

No comments:

Post a Comment