KESI YA JACOB ZUMA IMEHAIRISHWA. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Friday 6 April 2018

KESI YA JACOB ZUMA IMEHAIRISHWA.

kesi ya Rushwa inayo mkabili aliye kuwa Rais wa Africa kusini Jacob Zuma imehairishwa mpaka juni 8 2018 itakapo somwa tena.

Jacob Zuma alifika mahakama kuu ya Durban leo asubuhi kusikiliza kesi yake ambayo ina mashtaka 16, yakiwemo ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka na utakatishaji wa fedha.
Wafuasi wa Zuma walijikusanya maeneo ya karibu ya mahakama hiyo huku wakiimba nyimbo za kumsifu, wakisema hawatamuacha mpaka mwisho, na wengine wakikikesha kumuombea.
Kesi hiyo dhidi ya Zuma ilishwahi kufunguliwa na kusikilizwa, kisha kufutwa mwaka 2009, lakini sasa imeanza kusikilizwa tena baada ya kuondolwa madarakani, huku Rais aliyechukua wadhifa huo Cyril Ramaphosa akiahidi kukomesha vitendo vya rushwa nchini humo.

No comments:

Post a Comment