AUNTY EZEKIEL AJIBU TUHUMA ZA KUAZIMA NGUO KWA WEMA SEPETU. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Monday 2 April 2018

AUNTY EZEKIEL AJIBU TUHUMA ZA KUAZIMA NGUO KWA WEMA SEPETU.

Mwanadada Aunty Ezekiel amefunguka na kujibu tuhuma zilizokuwa zikimkabili kuhusu tabia yake ya kuazima nguo kwa rafiki yake wa karibu Wema sepetu , tuhuma ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao kila kukicha.

Aunty Ezekiel  amesema kuwa nguo wanayosema ameazima zilishonwa mbli na yeye ndiye  aliyekuwa wakwanza  kuvaa nguo hiyo lakini anashangaa sana watu wanapokuja na kumtuhumu kuhusu swala hilo.

Hata hivyo Aunty anasema kuwa bado kwao sio shida kuvaliana nguo kwa sababu ni marafiki hivyo ni swala la kawaida.

"Kwanza kuazima nguo sio shida kwetu kwa sababu ni rafiki yangu lakini cha ajabu ni kwamba nguo wanayoizungumzia wao zimefanana wala hakuna aliyenda kugonga hodi kwa mwenzake."-Alijibu Aunty

Wawili hao wamekuwa marafiki kwa muda mrefu sasa ingawa hapo katikati walikuwa wakionekana kutokuwa pamoja lakini sasa ivi mapenzi yamerudi na kuwa mapya kabisa. 

No comments:

Post a Comment