Mzee Akilimali aingilia ishu ya Chirwa - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Thursday 11 January 2018

Mzee Akilimali aingilia ishu ya Chirwa

 MWENYEKITIwa Barazala Wazeewa Yanga, Ibrahim Akilimali amemtetea mshambuliaji wakimataifawa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa kufuatia kukosa penalti katika mechi ya juzi dhidi ya URA ya UgandakwenyeKombe la Mapinduzi.

Yanga iliondolewa katika nusu fainalikwa penalti5-4 ambapo Chirwa alikosa kwaupande wa Yanga nakusababisha kuwa gumzo kutokanana tukio hilo.

 Akizungumza Akilimali alisema Chirwa hakufanya makosa katikakupiga penalti ya mwisho kwani alidhamiria kufunga nakilichotokea ni bahati mbaya na kudai kuwa, kochandiyeanayepaswa kulaumiwakutokanana kumtumialicha ya kutokuwa namazoezi ya pamojana wenzake.

“Yanga tumetolewa kiume katikamichuano ya Mapinduzi kwani hadi tunatoka tumefanikiwa kufanya vyema hadi dakika 90lakini kili­ chotokea hakipaswi kulaumiwa mchezaji.

“Timu ilichezavizuri ilipamba­ nanahatimaye kuweza kufikia hapo tulipofikiana ilikuwa ni lazimatimu moja isonge mbele.

“Siwezi kumlaumu Chirwa, kilichotokea ni bahati mbaya kwani, hata wachezaji wazuri Ulaya wanakosa penalti sembuseyeye, anayepaswa kulaumiwani kochakwanini amemchezesha mchezaji akiwa hanamazoezi, naona anayarudiayaleyale ya Kocha Hans Pluijm,” alisema Akilimali.

No comments:

Post a Comment