Odama afunguka ishu nzima kuhusu kujitenga - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Monday 6 November 2017

Odama afunguka ishu nzima kuhusu kujitenga

Jennifer Kyaka ‘Odama’.
MSANII wa filamu mwenye uwezo mkubwa awapo mbele ya kamera, Jennifer Kyaka ‘Odama’, amepangua ishu ya kuonekana anajitenga na wasanii wenzake ambapo kila mara anaonekanakivyakevyake tofauti na wasanii wengine.

Odama ameiambia Kilinge kuwa yeye haamini kama anajitenga lakini kuna wakati ni lazima afanye kazi zake, kwa maana siyo rahisi kila muda kukutana kama ilivyozoeleka huko nyuma, kwani maisha yamebadilika sana, ni lazi m a wakutane kwenye kitu maalum.

“Unajua watu hawaelewi tu, mtu anapobadili mfumo kidogo wanasema ameanza kujitenga, kitu ambacho siyo kweli, wakati wa sasa hakuna sababu ya kukutana kila mara, maana kuna vitu vingine vinakuwa haviendi kabisa tukiwa tunajikusanya " alisema Odama

No comments:

Post a Comment