CHIRWA AMPA JEURI NIYONZIMA YANGA. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Friday 15 September 2017

CHIRWA AMPA JEURI NIYONZIMA YANGA.

KUREJEA kwa mshambuliaji mwenye nguvu na kasi Mzambia, Obrey Chirwa kumempa jeuri ya kufanya vizuri beki wa kati wa timu hiyo, Kelvin Yondani katika mechi zao za Ligi Kuu Bara.
Mzambia huyo, alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu huku akikosa michezo miwili ya ligi kuu kabla ya mchezo wa Njombe Mji kutokea benchi dakika za mwishoni akichukua nafasi ya Donald Ngoma.
Beki wa kati wa timu hiyo, Kelvin Yondani.
Chirwa alikuwa nje ya uwanja akiwa anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja, aliukosa mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba uliomalizika kwa Yanga kufungwa kwa penalti.
Akizungumza  Yondani alisema Chirwa ni kati ya washambuliaji anaowakubali kutokana na aina yake ya uchezaji mbele ya wapinzani wao. Yondani alisema
Chirwa si mwoga mbele ya mabeki wakorofi na wakati wote anajiamini, hivyo anaamini kurejea kwake kutaimarisha safu yao ya ushambuliaji inayoongozwa na Ngoma na Ibrahim Ajibu.
“Binafsi namkubali sana Chirwa na siku zote akiwepo yeye uwanjani basi ninakuwa na matumaini makubwa ya ushindi.
“Chirwa ni mchezaji anayejiamini na siyo mwoga kwa mabeki akiamua jambo lake, huyu ni aina ya washambuliaji ninaowakubali kiukweli. “Angekuwepo katika mechi ya Ngao ya Jamii (dhidi ya Simba) naamini tungefanya vizuri,” alisema Yondani. Katika mechi hiyo ya Ngao ya Jamii, Yanga ilifungwa kwa penalti 5-4 baada ya kutoka suluhu.


No comments:

Post a Comment