RAMMY GALIS AHAIDI FUNGU HILI KWA MTOTO WA MASOGANGE - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Tuesday 15 May 2018

RAMMY GALIS AHAIDI FUNGU HILI KWA MTOTO WA MASOGANGE

Muigizaji wa filamu bongo Rammy Galis ambaye aliwahi kuwa kwenye mahusiano na video vixen Agness Gerald aliyefariki hivi karibuni, amekusudia kumpa fungu la pesa Sania mabye ni mtoto wa Agness aliyemuacha, mara baada ya kuzindua filamu yake aliyoigiza naye.
Akizungumza Rammy amesema kiasi hiko cha pesa atahakikisha anakamkabidhi mwenyewe mtoto Sania, ambayo ni stahiki yake kutokana na kazi aliyoifanya marehemu mama yake kwenye filamu ya 'Hukumu' waliyoigiza.
“Kwanza nisingependa kutangaza rasmi kiasi ambacho kitamfikia kwa sababu sijui filamu mauzi yake yatakuwaje, lakini mimi kama Ramy Galis nitatoa kile ambacho Mungu atanibariki kupitia filamu hii, kutakuwa na asilimia kadhaa ambazo nitaziweka kwa niaba ya mtoto, na nitakaa chini na famlia ya mtoto wa pande zote mbili watakapokubaliana na sio nibaki nazo mimi, ni haki ya yule mtoto”, amesema Rammy Galis.
Sambamba na hilo Rammy Galis amesema filamu hiyo anakusudia kufanya uzinduzi wake mkoani Mbeya ambako Agness ametokea, na anasubiri msiba upite kabisa ili watu wasije wakasema amefuata kiki ya msiba kufanya kazi zake.

No comments:

Post a Comment