KWANGWARU YA HARMONIZE YAKIMBIZA CHATI BBC TOP 5 - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Monday 7 May 2018

KWANGWARU YA HARMONIZE YAKIMBIZA CHATI BBC TOP 5

Harmonize amefanikiwa kuingiza ngoma yake ya Kwa Ngwaru kwenye Top 5 za Afro Boss Airline DNA za kipindi cha Destination Africa kinachoendeshwa na DJ Edu kupitia BBC Radio One Xtra.

Wimbo huo umefanikiwa kushika namba mbili kwenye chati hizo wakati namba moja ikishikiliwa na Davido kupitia wimbo wake mpya wa Assurance.

Wiki iliyopita wimbo huo ulishika namba tano kwenye chati hizo.

Wasanii wengine walioingia kwenye chati hizo ni Shado Chris (Kitadi), Bils na Giggz (Loudah) na Da Capo (Take It All). 

No comments:

Post a Comment