AZAM FC YATANGAZA KIAMA.. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Thursday 5 April 2018

AZAM FC YATANGAZA KIAMA..

Baada ya timu ya Azam kutolewa katika michuano ya kombe la shirikisho hivi karibuni na Mtibwa Sugar wamefunguka kudai kwa sasa silaha zao wanazikita kwenye ligi kuu ili waweze kuimarika kwa kujiweka katika nafasi nzuri katika mashindano hayo.

Hayo yamebainishwa na Afisa Habari wa Klabu hiyo, Jaffar Idd wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam kuelekea mchezo wao dhidi ya Mbeya City unaotarajiwa kuchezwa siku ya Jumapili (Aprili 8, 2018) katika dimba la Sokoine.
"Tunakwenda kupambana kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunacheza na kupata pointi tatu muhimu ili tuzidi kuimarika katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Sisi kama Azam FC tumeanza mazoezi tokea siku ya Jumatatu kwa ajili ya kujiweka sawa katika mchezo huo, tunajua utakuwa mchezo wenye ushindani na mgumu lakini tutahakikisha tunafanya vizuri", amesema Jaffar.
Kwa upande mwingine, timu ya Azam FC wanatarajia kuondoka leo (Ijumaa) kuelekea mkoani Mbeya tayari kwa mchezo huo 

No comments:

Post a Comment