Sanchi:awatolea povu hili wanao disi miguu yake - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Thursday 9 November 2017

Sanchi:awatolea povu hili wanao disi miguu yake

Jane Rimoy ‘Sanchi’.
MWANAMITINDO maarufu Bongo, Jane Rimoy ‘Sanchi’ amewatolea uvivu watu wanaomponda mitandaoni kuwa ana miguu mibaya akidai si kweli na watu hao wanasumbuliwa na wivu.

Akizungumza  Sanchi alisema kuwa ameona watu wengi wakichambua miguu yake kwenye mitandao ya kijamii lakini anaamini kwa vile wao hawana miguu kama yake ndio maana wanaichambua.

“Najua tatizo la Wabongo kama kitu wao hawawezi kukipata basi wanasingizia kitu hicho ni kibaya sasa hata ukiangalia miguu yangu ina tatizo gani kama si wivu unawasumbua tu, waende huko,” alisema Sanchi.

No comments:

Post a Comment