Ebitoke:Sijapotea kwenye game - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Monday 13 November 2017

Ebitoke:Sijapotea kwenye game

Anna Exavery ‘ Ebitoke’
UNAMKUMBUKA msanii wa vichekesho aliyejichukulia umaarufu mkubwa kwenye mitandao ya kijamii, Anna Exavery ‘ Ebitoke’, amedai kuwa bado hajapotea kwenye gemu kama wengine wanavyodhani.

Akizungumza Ebitoke alisema kuwa, si rahisi kwa yeye kupotea kwenye gemu kwa sababu amezaliwa kuchekesha, ana madude ya hatari ingawa kwa sasa yuko kwenye majukumu mengine.

“Ha ha ha haaa! Siyo rahisi kupotea kihivyo kama watu wanavyodhani, niko na madude ya hatari sijayaachia, sema kuna majukumu mengine ya kikazi nayafanya,”alisema Ebitoke

No comments:

Post a Comment