Mazoezi ya Simba balaa,wamepania kombe la Mapinduzi - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Sunday 7 January 2018

Mazoezi ya Simba balaa,wamepania kombe la Mapinduzi

Kikosi cha Simba kilichopo chini ya Kocha Masoud Djuma, kinaendelea na mazoezi jioni ya leo Jumapili kwenye Uwanja wa Nyuki, Zanzibar.

Simba jana walipoteza mechi dhidi ya Azam FC katika hatua ya makundi na ili kusonga mbele wanatakiwa kuwafunga URA.

Wachezaji wa Simba walionekana wakifanya mazoezi makali katika Uwanja wa Nyuki ili kuhakikisha wanajiweka fiti kwa ajili ya mchezo wa kesho Jumatatu.

Hata hivyo, Simba wana nafasi ya kusonga mbele huku wakitakiwa kuibuka na ushindi mbele ya Waganda hao ambao mchezo wao wa hivi karibuni waliifunga Azam FC.

No comments:

Post a Comment