SHAMSA FORD : FAIZA NI MKURUPUKAJI SANA.. - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Wednesday 11 April 2018

SHAMSA FORD : FAIZA NI MKURUPUKAJI SANA..

Jana April 10,2018 muigizaji Shamsa Ford amezungumza  na kufunguka kuhusu Faiza Ally kwa kile ambacho alikisema juu yake kuhusu madili makubwa wanayopata wanawake wa nje ndani ya Tanzania .

Kuna kipindi kama waliotoleana mapovu kupitia mtandao wa Instagram kuhusu ujio wa Zari na kusaini mkataba na moja kati ya kampuni jambo ambalo liliumiza vichwa vya mastaa wengi wa kike bongo huku wengine wakilaumu kwanini mikataba mizuri kama hiyo wanasaini watu wa njee na sio wazawa mmoja wapo akiwa Faiza.

Shamsa Ford amefunguka na kusema kuwa yeye na Faiza ni marafiki sana kuhusu kutofautiana ni kila mtu cha msingi ni kuheshimu mawazo ya mwenzio kwani alichokisema yeye kina maana kwa upande wake na kuona kinafaa na Mimi pia nina mtazamo wangu, alisema Shamsa Ford.

Jambo lingine ambalo ameongeze ni kwamba faiza ni
Mkurupukaji ila hashangai kwani inawezeka kuwa ni stress maana yeye ni single mama kwaiyo na yeye ana elewa hiyo situation.

No comments:

Post a Comment