Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Mil 1.5 Video Queen maarufu bongo , Agnes Gerald 'Masogange' katika kesi ya kutumia dawa za kulevya .
Masogange amepewa hukumu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.
Agness ni moja ya wasanii waliotajwa kwenye orodha ya Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda mwaka jana kwa kutuhumiwa kujihusisha na biashara pamoja na matumizi ya dawa za kulevya.
No comments:
Post a Comment