Sihitaji Mwanaume wa kunioa : Sanchi... - Erick Picson Media

Erick Picson Media

Mkali wa Matukio na Habari za Burudani

Breaking

Sunday 4 March 2018

Sihitaji Mwanaume wa kunioa : Sanchi...

 MWANA-MITINDO maarufu Bongo, Jane Ramoy ‘Sanchi’ ametoa la moyoni kuwa hahitaji mwanaume wa kumuoa kwa hivi sasa na kama angetaka, wapo wengi wamepanga msururu.

Mrembo huyo amefunguka hayo baada ya mitandao ya kijamii hivi karibuni kumuandama kuwa, iweje yeye ana ‘mzigo wa haja’ haolewi wengine ambao hawana hata shepu wanaolewa kila kukicha.

Kufuatia maneno hayo mtandaoni huku wengine wakipingana nayo kwa kusema siyo kila mwenye shepu ana haki ya kuolewa, Sanchi alisema:

“Jamani naomba watu wajue kabisa mimi sihitaji kuolewa kwa sasa, ningekuwa nataka kuolewa ingekuwa zamani, wapo wanaume wengi wanataka kuleta posa kwetu lakini sasa hivi nimesema hapana kwanza.”

No comments:

Post a Comment